Hali purukushani imeshuhudiwa Leo wakati wa mkutano wa wajumbe wa Chama Cha UDA kwenye kaunti ya Mombasa baada ya wafuasi wa mbunge wa EALA Hassan Omar Sarai na wale wa Mbunge wa Nyali Mohammed Ali kuonyeshana ubabe wa kisiasa.
NYOTA SULEIMAN
Jun 24, 2023
Ghasia zatanda kwenye mkutano wa UDA Mombasa
Hali purukushani imeshuhudiwa Leo wakati wa mkutano wa wajumbe wa Chama Cha UDA kwenye kaunti ya Mombasa baada ya wafuasi wa mbunge wa EALA Hassan Omar Sarai na wale wa Mbunge wa Nyali Mohammed Ali kuonyeshana ubabe wa kisiasa.
AFUENI KWA MADEREVA WA TUK TUK MOMBASA
Na Nyota Suleiman
MADEREVA wa Tuk Tuk katika kaunti ya Mombasa wana kila sababu ya kutabasamu baada ya kampuni ya Car General Kuzindua rasmi aina mpya za Tuk Tuk PIAGGIO NXT zenye Muundo wa kipee ambazo zinatarajiwa kupiga Jeki biashara hiyo na kuiboresha zaidi katika kaunti hiyo.
Uzinduzi wa aina hiyo mpya ya Tuk Tuk unajiri kufuatia malalamiko kutoka kwa madereva wa Tuk Tuk kuhusiana na mapungufu yaliyoshuhudiwa katika Tuk Tuk za hapo awali zilizonunuliwa kutoka kwa kampuni hiyo.
Kulingana na raisi wa Muunganao wa madereva wa Tuk Tuk kaunti ya Mombasa ambaye pia ni mwanzilishi wa biashara hiyo katika kaunti hiyo Chrispine Obondo maarufu Mr Dubai ameutaja uzinduzi huo kama hatua muhimu katika sekta ya uchukuzi katika kaunti ya Mombasa akisema itawasaidia pakubwa madereva wa Tuk Tuk kumudu gharama ya biashara hususan bei ya mafuta kutokana na muundo wa Kipekee wa Tuk Tuk Hizo.
Wakati huo huo ameipongeza kampuni ya Car and general kwa kutoa kipaumbele katika kuangazia maslahi na matatizo yanayowakumba Madereva na kutafuta suluhu muafaka ili Kuwawezesha kuendeleza biashara bila madhila yoyote.
Aidha ametoa wito kwa madereva wa Tuk Tuk katika kaunti ya Mombasa kupewa mafunzo ya Kutosha kuwawezesha kuendeleza shughuli zao ipasavyo ili kuwaepushia mahangaiko wanayopitia kutoka kwa maafisa trafiki katika kaunti hiyo.
Wakati huo huo ameonyesha kusikitishwa kwake na jinsi baadhi ya maafisa hao wa trafiki wamekuwa wakiwahanagaisha madereva wa tuk tuk bila hatia ,akiwataka kukomesha hujuma dhidi yao.
Baadhi ya Madereva waliyozungumza katika hafla ya Uzinduzi huo iliyoandaliwa katika uga wa Makadara mjini Mombasa Wameonyesha furaha yao kutokana ujio wa Tuk Tuk hizo mpya huku wakiwarai wenzao kujiunga na miungano ya madereva ili wawaze kujinufaisha zaidi.
Kwa upande wao maafisa kutoka kampuni ya Car and general waliyohudhuria uzinduzi huo wamewahimiza madereva kujitokeza na kuchukua mikopo ya kununua Tuk Tuk hizo mpya ili waweze kujiendeleza zaidi kichumi.
Nov 24, 2022
AFUENI KWA MADEREVA WA TUK TUK MOMBASA
Na Nyota Suleiman
Madereva wa Tuk Tuk katika kaunti ya Mombasa wana kila sababu ya kutabasamu baada ya kampuni ya Car General Kuzindua rasmi aina mpya za Tuk Tuk PIAGGIO NXT zenye Muundo wa kipee ambazo zinatarajiwa kupiga Jeki biashara hiyo na kuiboresha zaidi katika kaunti hiyo.
Uzinduzi wa aina hiyo mpya ya Tuk Tuk unajiri kufuatia malalamiko kutoka kwa madereva wa Tuk Tuk kuhusiana na mapungufu yaliyoshuhudiwa katika Tuk Tuk za hapo awali zilizonunuliwa kutoka kwa kampuni hiyo.
Kulingana na raisi wa Muunganao wa madereva wa Tuk Tuk kaunti ya Mombasa ambaye pia ni mwanzilishi wa biashara hiyo katika kaunti hiyo Chrispine Obondo maarufu Mr Dubai ameutaja uzinduzi huo kama hatua muhimu katika sekta ya uchukuzi katika kaunti ya Mombasa akisema itawasaidia pakubwa madereva wa Tuk Tuk kumudu gharama ya biashara hususan bei ya mafuta kutokana na muundo wa Kipekee wa Tuk Tuk Hizo.
Wakati huo huo ameipongeza kampuni ya Car and general kwa kutoa kipaumbele katika kuangazia maslahi na matatizo yanayowakumba Madereva na kutafuta suluhu muafaka ili Kuwawezesha kuendeleza biashara bila madhila yoyote.
Aidha ametoa wito kwa madereva wa Tuk Tuk katika kaunti ya Mombasa kupewa mafunzo ya Kutosha kuwawezesha kuendeleza shughuli zao ipasavyo ili kuwaepushia mahangaiko wanayopitia kutoka kwa maafisa trafiki katika kaunti hiyo.
Wakati huo huo ameonyesha kusikitishwa kwake na jinsi baadhi ya maafisa hao wa trafiki wamekuwa wakiwahanagaisha madereva wa tuk tuk bila hatia ,akiwataka kukomesha hujuma dhidi yao.
Baadhi ya Madereva waliyozungumza katika hafla ya Uzinduzi huo iliyoandaliwa katika uga wa Makadara mjini Mombasa Wameonyesha furaha yao kutokana ujio wa Tuk Tuk hizo mpya huku wakiwarai wenzao kujiunga na miungano ya madereva ili wawaze kujinufaisha zaidi.
Kwa upande wao maafisa kutoka kampuni ya Car and general waliyohudhuria uzinduzi huo wamewahimiza madereva kujitokeza na kuchukua mikopo ya kununua Tuk Tuk hizo mpya ili waweze kujiendeleza zaidi kichumi.
Sep 15, 2022
ABDULSWAMAD AAPISHWA KUWA GAVANA MOMBASA
Hatimaye aliyekuwa mbunge wa Mvita Abdulswamad Shariff Nassir ameapishwa rasmi kuwa gavana mpya wa kaunti ya Mombasa katika sherehe aliyoandaliwa katika bustani ya Mama Ngina Water Front Mjini Mombasa.
Abdulswamad ambaye anachukua hatamu ya kuwa gavana wa pili wa kaunti hiyo kutoka kwa aliyekuwa gavana Ali Hassan Joho,amewashukuru wakaazi wa kaunti ya Mombasa kwa kumpa nafasi ya kuongoza kaunti hiyo huku akiahidi kuwahudumia wote bila ya kuwabagua.
Wakati huo huo Nassir amewarai waliyokuwa wapinzani wake wa kisiasa kwenye kinyang’anyiro cha kuwania kiti hicho kuzika tofauti zao za kisiasa kuungana naye katika safari ya kuiendeleza na kuibadilisha kaunti ya Mombasa kimaendeleo.
Hatahivyo akiwahutubia mamia ya wakaazi walijitokeza kushuhudia sherehe ya kuapishwa kwake, Nassir ameahidi kuwa uongozi wake utafanikisha Ugatuzi ipasavyo kwenye kaunti hiyo ili kuleta mageuzi ya kiuchumi na kutengeneza fursa za ajira kwa wakaazi.
Aidha Nassir amesema kuwa ndani ya siku mia moja za utawala wake atahakikisha kuwa huduma za serikali ya kaunti ya Mombasa zitapatikana kwa njia raisi kupitia mpango Huduma Mtaani ambao utabadilisha mchakato mzima wa kutafuta huduma kwenye kaunti hiyo.
Katika sekta ya afya Abdulswamad amebainisha kuwa serikali yake itaanzisha mpango wa afya care unaonuia kuwawezesha wakaazi kutoka familia maskini kwenye kaunti hiyo kupata huduma za matibabu wakati wanapokuwa wagonjwa.
wakati huo huo akisema kuwa watatoa nafasi za mafunzo kwa madaktari ilikuwawezsha kutoa huduma za kiwango cha juu.
Vile Vile Katika Sekta ya elimu amesema kuwa serikali yake itaweka mpango wa basari utakaowawezesha wanafunzi kusoma bila kufukuzwa shule kwa sababu ya karo. Mpango huo uliopewa jina la Elimu Fund unatarajiwa kuwawezesha wanafunzi kutoka familia maskini kuendeleza masomo bila tashwishi.
Aidha Nassir amewahakikisha wakaazi wa kaunti ya hiyo kuwa utawala wale utashughulikia tatizo la mrundiko wa taka kwenye kaunti hiyo akisema kuwa ndani ya siku mia moja za utawala wake wanatarajia kuanza zoezi la kuokota na kuchakata taka hizo ili kusafisha mazingira.
Miongoni mwa viongozi wa kuu wa n mrengo Azimio walijitokeza katika sherehe hiyo ni pamoja na Martha Karua pamoja na Kalonzo Musyoka.
Aug 19, 2022
SABABU ZA RUTO KUIMARIKA PWANI KATIKA UCHAGUZI MKUU
Licha ya kuwa mgombeaji wa kiti Cha Urais Kupitia Muungano wa Azimio One Kenya Raila Odinga amefanikiwa kwa mara nyengine tena kuibuka na kura nyingi katika kanda wa pwani katika
uchaguzi mkuu uliyotamatika, rais mteule William Ruto kwa upande wake amefanikiwa
kupunguza pengo lilokuwa hapo awali na imani kuwa kuwa kanda ya pwani ni ngome ya kisiasa ya Bwana Odinga.
Ruto pamoja na timu yake ya Kampeni walitumia
mikakati amabayo iliwawezesha kupata kura takriban laki 336,478 katika kaunti sita za
pwani amabzo zinajumuisha ile ya Mombasa,
Lamu, Tana River, Kwale, Kilifi and Taita Taveta. Hesabu hiyo ikiwa ni Ongezeko
kutoka Kura hizo ikiwa ni Ongezeko kutoka kura 287,606 ambazo chama cha Jubilee kulifanikiwa
kupata katika uchaguzi wa mwaka 2017 ambao uliwapa ushindi rais Uhuru Kenyatta
pamoja na Ruto.
Wadadisi
wa maswala ya kisiasa wanahoji kuwa Ongezeko la Kura alizozipata Bwana Ruto
Katika kanda ya Pwani zinatokana na hatua
yake ya kuwavuta Viongozi tajika wa eneo
hilo upande wake pamoja na kuandaa vikao vya kujadili maswala ya maendeleo eneo
hilo ili kuwavutia wapiga kura kujifungamanisha na chama chake cha UDA.
Aug 18, 2022
SARAI AIKOSOA IEBC KUHAIRISHA UCHAGUZI WA UGAVANA
Mgombeaji wa kiti cha Ugavana katika kaunti ya
Mombasa kupitia kwa chama cha UDA Hassan Omar Sarai ameikosoa tume huru ya
Uchaguzi na Mipaka nchini IEBC kufuatia hatua yake hapo Jana kuahirisha tena
uchaguzi wa Ugavana katika kaunti hiyo.
Akizungumza katika kikao na wananahabari mjini
Mombasa,Sarai ameitaja hatua hiyo ya IEBC kama inayoongeza hofu miongoni mwa
wakaazi wa kaunti hiyo huku akimtaka mwenyekiti wa time hiyo wafula Chebukati kuweka
tarehe kamili ambapo uchaguzi huo utaandaliwa.
Wakati huo huo Sarai amewatahadharisha maafisa wa
usalama dhidi ya Kutumiwa vibaya na baadhi ya wanasiasa,akisema kuwa licha ya
Maafisa hao kuwahujumu, kamwe hawatalipiza kisasi huku akiwataka kutekeleza
majukumu yao kulingana na katiba.
Kwa upande Mgombea mwenza wa Sarai katika
kinyang’anyiro hicho Selina Maitha amewatolea wito wakaazi wa Mombasa kujitokeza
kwa wingi siku ya kupiga kura na kuwapa fursa ya kuongoza kaunti hiyo Ili kuleta
mageuzi ya Kimaendeleo.
Mar 10, 2022
SERIKALI KUIMARISHA USALAMA BAHARINI
Serikali ya kitaifa imejikita katika kuunda mkakati
wa kitaifa wa usalama wa baharini unaonuia kukabiliana na changamoto za kiusalama
zinazotokana na shughuli za uchumi samawati. Mkakati huo utakaohusisha
kamati ya kitaifa ya Usalama wa baharini na sajili ya sajili ya kitaifa ya
usalama wa baharini, ni mkakati wa kisera utakaojumuisha malengo na ruwaza ya
kuimarisha usalama wa majini katika taifa hili .
Akizungumza mjini Mombasa katika warsha ya ufunguzi wa mkakati huo ,katibu wa kudumu
katika idara ya taifa ya maswala ya Afrika Mashariki daktari Kevit
Desai,amesema kuwa mkakati huo umeundwa ili kurahisisha ushirikiano baina ya wadau pamoja na uangalizi
wa hatari na vitisho katikia sekta ya shughuli za baharini.
Aidha Desai
amebainisha kuwa uchumi samawati unashikilia nafasi ya nane miongoni mwa
mihimili ya kiuchumi katika ruwaza ya mwaka 2030 na ya tatu katika agenda nne
kuu za serikali,akisema kuwa taifa hili taifa hili limejiandaa vilivyo katika
kutekeleza jukumu muhimu la kuhakikisha usalama katika bahari hindi.
Wakati huo huo amesema kuwa ipo haja ya kulinda
usalama wa majini kutokana na vitisho vya ndani na nje ya nchi ili kuruhusu
usafirishaji wa watu na mizigo ufanyike kwa njia ya amani kwani unachangia biashara kwa asilimia tisini katika
ukanda huu.
Mar 2, 2022
MOMBASA ILIVYOATHIRIKA NA VITA NCHINI UKRAINE
Na Nyota Suleiman.
Mzozo unaoendelea hivi sasa baina ya Mataifa ya Ukraine na Urusi bila shaka umesababisha athari ya Moja kwa moja kwa Kaunti ya Mombasa.Mnamo mwaka jana serikali ya Kaunti ya Mombasa iliingia makubaliano ya ushirika na upatanisho wa kibiashara baina ya serikali na wadau binafsi katika miji ya Odes na Kiev katika taifa la Ukraine.
Utawala wa Gavana wa kaunti ya Mombasa Ali Hassan Joho Ulituma UJumbe kuelekea nchini Ukraine Ili kufanya ziara iliyolenga kujenga uhusiano mwema baina ya kaunti ya Mombasa na taifa hilo la Ukraine.Aidha baada ya ziara hiyo ujumbe kutoka taifa la Ukraine nao pia uliwasili katika kaunti ya Mombasa kukagua sehemu za vivutio vya watalii ambavyo vinapatikana katika kaunti ya Mombasa na pwani ya Kenya kwa Ujumla.
Makubaliano hayo ya ushirika yaliifanya kaunti ya Mombasa kuanza kupokea Ndege kadhaa za watalii zilizoidhinishwa kutoka taifa la Ukraine katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Moi.
Aidha Mapema Mwezi wa Februari Mwaka huu Serikali ya kaunti ya Mombasa iliingia katika mkataba mwengine na taifa hilo la ambao ungewezesha wataalamu mbalimbali na madaktari katika kaunti ya Mombasa kupata mafunzo katika taifa hilo la Ughaibuni.Hata hivyo vita vinavyoendelea hivi sasa katika Taifa hilo vimeufanya mpango huo kusimama huku hatima yake bado ikiwa haijulikani.Kulingana na Afisa mkuu wa Afya kaunti ta Mombasa daktari Khadija Shikely kundi la kwanza la madaktari hao lilitarajiwa kusafiri nchini Ukraine mwanzoni mwa mwezi Machi.
Mbali na Ushirikiano katika sekta ya Matibabu Taifa la Ukraine limekuwa likishirikiana na Kaunti ya Mombasa katika kukuza utalii lakini kutokana na kuzuka kwa vita hatima ya makubaliano hayo ya Ushirika kwa sasa haijulikani .
Feb 25, 2022
DARAJA LA MAKUPA KUANZA KUTUMIKA JUNI
NA NYOTA SULEIMAN
Halmashauri ya barabara kuu za Kenya KENHA Imesema kuwa
daraja la Makupa lilogharimu jumla ya
shilingi bilioni 4.5 linatarajiwa kuanza
kutumika mwezi juni mwaka
huu.Daraja hilo ambalo ujenzi wake ulianza mwezi Aprili mwaka jana kwa sasa
limekamilika kwa asilimia hamsini na saba.
Aidha Kulinagana na Mhandisi mkaazi wa mradi huo Stephen Gicheru ni kwamba awali mradi huo
ulitarajiwa kukamilika ndani ya miezi kumi na mbili lakini kutokana na kucheleshwa kwa kazi
muhimu katika ujenzi huo kuliwalazimu kutathmini upya muda wa kuukamilisha .
Gicheru pia ameongezea kuwa ipo mipango ya kuiondoa barabara
ya Makupa Courseway baada ya kukamilika kwa daraja hilo lakini hilo huenda
likachukua muda zaidi.
Wakati huo huo
amesema kuwa wanatarajia daraja hilo litaanza kutumika punde tu baada ya kukamilika kwake ,huku kazi nyengine
zilizosalia zikiendelezwa huku likitumika .Kandarasi ya kulikarabati daraja hilo lenye urefu wa
mita 457 ambalo litaunganisha eneo la Tudor na port reitz ilipewa kampuni ya China Construction
Coporation mwezi novemba mwaka 2020.
Feb 18, 2022
KAMPUNI YA PEPSI YAFUNGUA BOHARI MOMBASA
Ushindani katika sekta ya utengenezaji wa vinywaji nchini unatarajiwa kuongezeka kufuatia hatua ya kampuni maarufu duniani inayojishuguhulisha na utengenezaji wa vinywaji ya Pepsi kuzindua bohari katika kaunti ya Mombasa, huku kampuni hiyo ikilenga kupenyeza katika soko la ukanda wa Afrika Mashariki.
Akizungumza wakati wa kuzinduliwa kwa bohari hilo katika kaunti ya Mombasa ,Afisa anayelisimamia salim Oganda amesema kuwa kampuni ya Pepsi kwa miaka mingu imetamani kupanua wigo wake katika ukanda wa pwani kutokana na udhabiti wa soko lake eneo hili.
Aidha Ameongezea kuwa kwa sasa kampuni hiyo inalenga soko la pwani ya Kenya baada ya kufungua maduka katika kaunti za Kisumu na Nairobi akiongezea kuwa kufikia sasa zaidi ya watu arubaini wameajiriwa na wengine zaidi wakitarajiwa kuajiriwa katika siku za usoni.
Kwa upande wake Mbunge wa Mvita Abdulswamad Sharif Nassir ambaye alihudhuria uzinduzi huo amewarai wawekezaji kuekeza katika ukanda wa pwani kutokana na ukuaji wa utalii katika eneo hili huku akiitolea wito serikali kutathmini upya ushuru unaowekewa wawekezaji wapya wa wakigeni.
HIVI PUNDE
Ghasia zatanda kwenye mkutano wa UDA Mombasa
Hali purukushani imeshuhudiwa Leo wakati wa mkutano wa wajumbe wa Chama Cha UDA kwenye kaunti ya Mombasa baada ya wafuasi wa mbunge wa EALA...
-
NA NYOTA SULEIMAN MOHAMED Viongozi mbalimbali wamekuwa mstari wa mbele kuwahimiza wananchi kujiandikisha kama wapiga kura kabla la zoezi k...
-
Aliyekuwa Mwaniaji wa Kiti cha ugavana kaunti ya Mombasa Suleiman Shahbal amekihama chama cha Jubilee na kuregea katika chama Cha ODM huku u...
-
Na Nyota Suleiman MADEREVA wa Tuk Tuk katika kaunti ya Mombasa wana kila sababu ya kutabasamu baada ya kampuni ya Car General Kuzindua rasm...





