Feb 25, 2022

DARAJA LA MAKUPA KUANZA KUTUMIKA JUNI

 NA NYOTA SULEIMAN

Halmashauri ya barabara kuu za Kenya KENHA Imesema kuwa daraja la Makupa  lilogharimu jumla ya shilingi bilioni 4.5 linatarajiwa kuanza  kutumika mwezi  juni mwaka huu.Daraja hilo ambalo ujenzi wake ulianza mwezi Aprili mwaka jana kwa sasa limekamilika kwa asilimia hamsini na saba.


Aidha Kulinagana na Mhandisi mkaazi wa mradi huo  Stephen Gicheru ni kwamba awali mradi huo ulitarajiwa kukamilika ndani ya miezi kumi na mbili  lakini kutokana na kucheleshwa kwa kazi muhimu katika ujenzi huo kuliwalazimu kutathmini upya muda wa kuukamilisha .

Gicheru pia ameongezea kuwa ipo mipango ya kuiondoa barabara ya Makupa Courseway baada ya kukamilika kwa daraja hilo lakini hilo huenda likachukua muda zaidi.

Wakati huo huo  amesema kuwa wanatarajia daraja hilo litaanza kutumika punde tu  baada ya kukamilika kwake ,huku kazi nyengine zilizosalia zikiendelezwa huku likitumika  .Kandarasi  ya kulikarabati daraja hilo lenye urefu wa mita 457 ambalo litaunganisha eneo la Tudor na port reitz ilipewa kampuni ya China Construction Coporation mwezi novemba mwaka 2020.

 

HIVI PUNDE

Ghasia zatanda kwenye mkutano wa UDA Mombasa

Hali purukushani imeshuhudiwa Leo wakati wa mkutano wa wajumbe wa Chama Cha UDA kwenye kaunti ya Mombasa baada ya wafuasi wa  mbunge wa EALA...