Na Nyota Suleiman.
Mzozo unaoendelea hivi sasa baina ya Mataifa ya Ukraine na Urusi bila shaka umesababisha athari ya Moja kwa moja kwa Kaunti ya Mombasa.Mnamo mwaka jana serikali ya Kaunti ya Mombasa iliingia makubaliano ya ushirika na upatanisho wa kibiashara baina ya serikali na wadau binafsi katika miji ya Odes na Kiev katika taifa la Ukraine.
Utawala wa Gavana wa kaunti ya Mombasa Ali Hassan Joho Ulituma UJumbe kuelekea nchini Ukraine Ili kufanya ziara iliyolenga kujenga uhusiano mwema baina ya kaunti ya Mombasa na taifa hilo la Ukraine.Aidha baada ya ziara hiyo ujumbe kutoka taifa la Ukraine nao pia uliwasili katika kaunti ya Mombasa kukagua sehemu za vivutio vya watalii ambavyo vinapatikana katika kaunti ya Mombasa na pwani ya Kenya kwa Ujumla.
Makubaliano hayo ya ushirika yaliifanya kaunti ya Mombasa kuanza kupokea Ndege kadhaa za watalii zilizoidhinishwa kutoka taifa la Ukraine katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Moi.
Aidha Mapema Mwezi wa Februari Mwaka huu Serikali ya kaunti ya Mombasa iliingia katika mkataba mwengine na taifa hilo la ambao ungewezesha wataalamu mbalimbali na madaktari katika kaunti ya Mombasa kupata mafunzo katika taifa hilo la Ughaibuni.Hata hivyo vita vinavyoendelea hivi sasa katika Taifa hilo vimeufanya mpango huo kusimama huku hatima yake bado ikiwa haijulikani.Kulingana na Afisa mkuu wa Afya kaunti ta Mombasa daktari Khadija Shikely kundi la kwanza la madaktari hao lilitarajiwa kusafiri nchini Ukraine mwanzoni mwa mwezi Machi.
Mbali na Ushirikiano katika sekta ya Matibabu Taifa la Ukraine limekuwa likishirikiana na Kaunti ya Mombasa katika kukuza utalii lakini kutokana na kuzuka kwa vita hatima ya makubaliano hayo ya Ushirika kwa sasa haijulikani .