Hali purukushani imeshuhudiwa Leo wakati wa mkutano wa wajumbe wa Chama Cha UDA kwenye kaunti ya Mombasa baada ya wafuasi wa mbunge wa EALA Hassan Omar Sarai na wale wa Mbunge wa Nyali Mohammed Ali kuonyeshana ubabe wa kisiasa.
Kizazaa kilizuka pale mbunge wa Nyali Mohamed Ali aliposhambuliwa na watu wanaodaiwa kuwa wafuasi wa Hassan Omar Sarai wakati alipowasili kwenye ukumbi wa mkutano huo, Hali iliyopekelea kurushwa kwa vitoza machozi na watu wasiojukikana ili kuutawanya umati uliyokuwa umejaa ukumbini humo.
Matukio hayo yalilazimu kuhairishwa kwa mkutano huo wa wajumbe ambao ulikuwa umeandakiwa kwa lengo la kuwahamasisha wanachama wa UDA kuhusiana na uchaguzi wa chama hicho unaotarajiwa kuandaliwa mnamo Mwezi Agosti pamoja na kujadiliwa kwa ajenda za chama.
Hatahivyo akihutubia wanahabari kuhusiana na matukio hayo Mbunge wa Nyali Mohammed Ali amemkosoa Hassan Omra sarai kwa madai ya kutumia vibaya nafasi yake kwenye chama UDA ili kuhujumu matokea ya uchaguzi unaotarajiwa kuandaliwa Mwezi Agosti.
Mbunge huyo amemtaka Sarai kujikita katika majukumu yake kama Mbunge wa Kenya kwenye bunge la Afrika Mashariki badala ya kujihusisha na siasa za chama hicho na kuleta migawanyiko.
Kwa upande wake Hassan Omar Sarai amemtuhumu mbunge huyo wa Nyali kwa madai ya kughushi kadi za wajumbe waliyoalikwa kuhudhuria mkutano huo akidai kuwa wengi wafuasi wake hakuwa wajumbe halisi wa UDA bali watu waliyokuwa na nia ya kuzua ghasia kwenye mkutano huo.
Wakati huo huo Sarai amepuuzilia mbali madai yaliyoibuliwa na mbunge hiyo yakumtuhumu kuwa na nia ya kuhujumu uchaguzi wa chama hicho huku akibainisha kama naibu mwenyekiti wa chama hicho hana nia ya kufanya hivyo.
Amekashifu ghasia zilizishuhudiwa wakati wa mkutano huo huku akipuuzilia mbali madai kuwa analenga kuhujumu uchaguzi wa chama hicho.
Naye katibu mkuu wa chama cha UDA Cleophas Malala ambaye alikuwa amehudhuria mkutano amesisitiza Kuwa uongozi wa chama hicho kamwe hautaegemea upande wowote katika uchaguzi unaokuja huku akiwataka viongozi hao wawili kukaa chini na kuzika tofauti zao.
Wakati huo huo amesema kuwa chama kitalazimika kuchukua hatua za kinidhamu kwa kiongozi yeyote atakayepatikana kuhisika na ghasia zilizishuhudiwa wakati wa mkutano huo.


