Feb 2, 2022

WAKAAZI WA CHANGAMWE WATAKIWA KUJISAJILI NA IEBC SAWIA NA CHAMA CHA ODM

 


NA NYOTA SULEIMAN MOHAMED

Viongozi mbalimbali wamekuwa mstari wa mbele kuwahimiza wananchi kujiandikisha kama wapiga kura kabla la zoezi kufungwa.

katika kaunti ya Mombasa Uongozi wa chama cha ODM  umefanya misururu ya mikutano katika eneo bunge la Changamwe ili kuwahamasisha wananchi   kujitokeza kwa wingi  na kujisajili kama wapiga kura pamoja kujiandikisha kuwa wanachama wa chama hicho.


 

Akiongoza msafara huo Mwenyekiti wa Chama cha ODM kaunti ya Mombasa Mohamed Khamid Khamis maarufu DEE amewarai wananchi katika eneo bunge hilo kujisajili kwa wingi  kama wapiga kura ili kumpeleka Ikulu  kinara wa Chama hicho Raila Odinga baada ya uchaguzi mkuu.


Aidha Mohamed ameendelea kusisitiza kuwa uteuzi wa chama hicho utafanyika kwa njia huru na haki,akiwahimiza wakaazi wa Changamwe kuchukua kura kwa wingi na kusajili katika chama cha  ODM , akisema kuwa ni  wale waliojisajili na chama pekee ndio watakao ruhusiwa kupiga kura katika kura za mchujo.

Kwa Upande wake katibu mkuu wa chama cha ODM kaunti ya Mombasa Geoffrey Busaka ameendelea kumpigia debe kinara wa chama hicho Raila Odinga akisema kwamba juhudi za kinara wa chama cha ODM Raila Odinga za kuingia ikulu zitategemea mno na kura za Wakaazi wa Kaunti nzima ya Mombasa.

HIVI PUNDE

Ghasia zatanda kwenye mkutano wa UDA Mombasa

Hali purukushani imeshuhudiwa Leo wakati wa mkutano wa wajumbe wa Chama Cha UDA kwenye kaunti ya Mombasa baada ya wafuasi wa  mbunge wa EALA...