Feb 18, 2022

KAMPUNI YA PEPSI YAFUNGUA BOHARI MOMBASA

 





Ushindani katika sekta ya utengenezaji wa vinywaji nchini  unatarajiwa kuongezeka kufuatia hatua ya kampuni maarufu duniani inayojishuguhulisha na utengenezaji  wa vinywaji ya Pepsi kuzindua bohari  katika kaunti ya Mombasa, huku kampuni hiyo ikilenga  kupenyeza  katika soko la ukanda  wa Afrika Mashariki.

Akizungumza  wakati wa kuzinduliwa kwa bohari hilo katika kaunti ya Mombasa  ,Afisa anayelisimamia salim Oganda amesema kuwa kampuni ya Pepsi  kwa miaka mingu imetamani  kupanua wigo wake  katika ukanda wa pwani kutokana na udhabiti wa soko lake eneo hili.

Aidha Ameongezea kuwa kwa sasa kampuni hiyo inalenga  soko la pwani ya Kenya baada ya kufungua maduka katika kaunti za Kisumu na Nairobi akiongezea kuwa  kufikia sasa zaidi ya watu arubaini wameajiriwa na wengine zaidi wakitarajiwa kuajiriwa katika siku za usoni.

Kwa upande wake Mbunge wa Mvita Abdulswamad Sharif Nassir ambaye alihudhuria uzinduzi huo amewarai wawekezaji kuekeza katika ukanda wa pwani kutokana na ukuaji wa utalii katika eneo hili huku akiitolea wito  serikali kutathmini upya ushuru unaowekewa  wawekezaji wapya wa wakigeni.

HIVI PUNDE

Ghasia zatanda kwenye mkutano wa UDA Mombasa

Hali purukushani imeshuhudiwa Leo wakati wa mkutano wa wajumbe wa Chama Cha UDA kwenye kaunti ya Mombasa baada ya wafuasi wa  mbunge wa EALA...