Aug 18, 2022

SARAI AIKOSOA IEBC KUHAIRISHA UCHAGUZI WA UGAVANA

 

Mgombeaji wa kiti cha Ugavana katika kaunti ya Mombasa kupitia kwa chama cha UDA Hassan Omar Sarai ameikosoa tume huru ya Uchaguzi na Mipaka nchini IEBC kufuatia hatua yake hapo Jana kuahirisha tena uchaguzi wa Ugavana katika kaunti hiyo.

Akizungumza katika kikao na wananahabari mjini Mombasa,Sarai ameitaja hatua hiyo ya IEBC kama inayoongeza hofu miongoni mwa wakaazi wa kaunti hiyo huku akimtaka mwenyekiti wa time hiyo wafula Chebukati kuweka tarehe kamili ambapo uchaguzi huo utaandaliwa.




Wakati huo huo Sarai amewatahadharisha maafisa wa usalama dhidi ya Kutumiwa vibaya na baadhi ya wanasiasa,akisema kuwa licha ya Maafisa hao kuwahujumu, kamwe hawatalipiza kisasi huku akiwataka kutekeleza majukumu yao kulingana na katiba.


Kwa upande Mgombea mwenza wa Sarai katika kinyang’anyiro hicho Selina Maitha amewatolea wito wakaazi wa Mombasa kujitokeza kwa wingi siku ya kupiga kura na kuwapa fursa ya kuongoza kaunti hiyo Ili kuleta mageuzi ya Kimaendeleo.


HIVI PUNDE

Ghasia zatanda kwenye mkutano wa UDA Mombasa

Hali purukushani imeshuhudiwa Leo wakati wa mkutano wa wajumbe wa Chama Cha UDA kwenye kaunti ya Mombasa baada ya wafuasi wa  mbunge wa EALA...