Wabunge wa bunge la kitaifa wanatishia kulemaza vikao vya bunge siku ya alhamisi wakati wa usomwaji wa bajeti ya kitaifa, kwa kile wanachodai ni uchekeshwaji wa usambazaji kwa pesa za ustawishaji wa maeneo bunge CDF.
Awali Mwezi machi mwaka huu waziri wa hazina ya kitaifa ukur yattani aliahidi kutoa shilingi bilioni 2 kila wiki hadi mwisho wa mwaka wa kifedha 2020/2021.
Kulingana na wabunge ahadi bado hiyo haijatimizwa.
Mwezi huo wa Machi aidha wabunge Waliikosoa hazina ya kitaifa wakiapa kuiangusha miswada ya serikali inayohusu hazina hiyo kama ingeshindwa kusambaza pesa hizo.
Hatahivyo ilibainika kuwa maeneo bunge 290 tayari yamepokea kiwango cha shilingi milioni 20 pekee kati ya milioni 137 kwa mwaka huu wa kifedha.