Jun 9, 2021

WABUNGE WATISHIA KUTATIZA USOMWAJI WA BAJETI ALHAMISI

Wabunge wa bunge la kitaifa wanatishia kulemaza vikao vya bunge siku ya alhamisi wakati wa usomwaji wa bajeti ya kitaifa,  kwa kile wanachodai ni uchekeshwaji wa usambazaji kwa pesa za ustawishaji wa maeneo bunge CDF. 

Awali Mwezi machi mwaka huu waziri wa hazina ya kitaifa ukur yattani aliahidi kutoa shilingi bilioni 2 kila wiki hadi mwisho wa mwaka wa kifedha 2020/2021.
Kulingana na wabunge ahadi bado  hiyo haijatimizwa. 

 Mwezi huo wa Machi aidha wabunge Waliikosoa hazina ya kitaifa wakiapa kuiangusha miswada ya serikali inayohusu hazina hiyo kama ingeshindwa kusambaza pesa hizo.

Hatahivyo ilibainika kuwa maeneo bunge 290 tayari yamepokea kiwango cha shilingi milioni 20 pekee kati ya milioni 137 kwa mwaka huu wa kifedha. 

HIVI PUNDE

Ghasia zatanda kwenye mkutano wa UDA Mombasa

Hali purukushani imeshuhudiwa Leo wakati wa mkutano wa wajumbe wa Chama Cha UDA kwenye kaunti ya Mombasa baada ya wafuasi wa  mbunge wa EALA...