Jun 11, 2021

WAZIRI YATANI AAINISHA SERA SABA ZA KUFUFUA UCHUMI.


Waziri wa hazina ya kitaifa Ukur Yatani amebainisha sera saba zilizopewa kipaumbele na serikali kwa ajili ya kufufua uchumi wa nchi kwa kasi kutokana na athari zilizoletwa na janga la Covid19.
 Akisoma taarifa ya bajeti ya mwaka 2021/2022,  Waziri Yatani alibainisha kuwa utekelezaji wa ajenda nne kuu za rais uhuru Kenyatta bado unabakia nyenzo muhimu ya kuufufua uchumi. 

Kutokana hilo, Waziri yatani amesema kuwa serikali itahakisha mipango na miradi chini ya ajenda nne kuu imewezeshwa. Miongoni mwazo ikiwa,  usalama wa chakula na lishe, Afya bora kwa wote, makaazi ya bei nafuu na ukuaji wa sekta ya viwanda/uzalishaji kwa ajiili ya kupunguza ukosefu wa ajira. 

Kufikia lengo hili ,waziri alidokeza kuwa serikali itachukua hatua za kimkakati zitakazo nuia kuhakikisha maendeleo endelevu ya kiuchumi Miongoni mwa hoja nyingine. 

HIVI PUNDE

Ghasia zatanda kwenye mkutano wa UDA Mombasa

Hali purukushani imeshuhudiwa Leo wakati wa mkutano wa wajumbe wa Chama Cha UDA kwenye kaunti ya Mombasa baada ya wafuasi wa  mbunge wa EALA...