Chama cha Mahakimu na majaji nchini (KMJA) na kile cha wanasheria (LSK) Kwa pamoja vimemkosoa rais Uhuru Kenyatta kwa kile wanachodai ni uteuzi wa majaji kibaguzi.
Haya yanajiri siku moja tu baada ya rais Uhuru Kenyatta kuwateuwa majaji waliyopendekezwa na tume ya huduma za mahakama (JSC) zaidi ya miaka miwili iliyopita. Hata hivyo cha kushangaza rais uhuru aliteuwa majaji 34 pekee na kukataa uteuzi wa majaji sita.
Katika taarifa kwa vyombo vya habari chama cha KMJA kimesema kuwa rais uhuru Kenyatta anawajibishwa kisheria Kuwateuwa majaji wote waliyopendekezwa na tume ya JSC.
Katibu mkuu wa chama cha KMJA amesema kuwa majina yanapopendekezwa na JSC kwa ajili ya uteuzi , rais hana wajibu wowote kisheria kufanya mabidiliko, kwani kufanya hivyo ni kuingilia uhuru wa tume hiyo
Aidha chama cha LSK kwa upande wake kimeongezea kuwa kitendo cha rais kushindwa kuteua majaji ndani ya siku 14 zilizoweka baada ya kupendekezwa na tume ya JSC ni ukiukaji wa sheria.