Jun 3, 2021

POLISI WANASA BUNDUKI NANE HARAMU NA RISASI KWA MWENZAO

Maafisa kutoka idara ya upelelezi DCI na wenzao kutoka idara ya polisi kituo cha Cherangani,  mnamo usiku wa jumanne walifanikiwa kupata bunduki nane kwa pamoja katika nyumba ya afisa wa polisi anayehudumu Nairobi. 

Kulingana na polisi kutoka kituo cha Cheranganyi, nyumba waliyoivamia ina milikiwa na Maxwell Tally Mutonyi ambaye ni afisa wa polisi dereva anayehudumu katika idara ya mahakama lakini anaishi katika makaazi ya maafisa wa polisi yaliyoko South B jijini Nairobi. Polisi wanasema kuwa alitoweka muda mfupi baada ya wao kuvamia nyumba yake.

Wakati wa msako huo maafisa wa polisi walifanikiwa kupata bunduki aina ya UZI SMG ikiwa na risasi S/No.  09234, smith na Wesson revolver S/No.38SPL, Six Germany Walther pistols S/Nos BE5768, XB3026, BP4957, AW5339, ME8395 na HJ6205  magazines, 197.pamoja na risasi nyengine. 
Afisa huyo wa polisi anatarajiwa kukamatwa na kufunguliwa mashtaka.

HIVI PUNDE

Ghasia zatanda kwenye mkutano wa UDA Mombasa

Hali purukushani imeshuhudiwa Leo wakati wa mkutano wa wajumbe wa Chama Cha UDA kwenye kaunti ya Mombasa baada ya wafuasi wa  mbunge wa EALA...