May 30, 2021

JAMII ZA WAFUGAJI ZATAKIWA KUKOMESHA VITA

Aliyekuwa mwenyekiti wa tume ya uwiano na utangamano Francis Ole Kaparo amewarai viongozi kutoka jamii za wafugaji kutafuta njia za kusuluhisha migogori iliyodumu kwa muda mrefu baina yao. 

Kaparo aliyaongea hayo alipokutana na viongozi kutoka jamii zinazozozana mara kwa mara za pokot na Samburu.Aliwasihi viongozi wa jamii hizo kutafuta suluhisho la kudumu ambalo litasaidia kumaliza mashambulizi ya kulipiza kisasi na wizi wa mifugo miongoni mwao. 

Aidha mwenyekiti huyo wa zamani wa NCIC alionyesha kusikitishwa kwake na jamii hizo mbili ambazo zimekuwa zikijuhusisha na mashambulizi ya kulipiza kisasi yanayosababisha wizi wa mifugo. 


Vile vile aliwashtumu baadhi ya viongozi wa jamii za wafugaji na wasomi kutoka kaunti za Laikipi, Samburu,Isiolo na Baringo kwa kushindwa kumaliza migogoro hiyo inayoendelea kuongezeka na ambayo imesababisha vifo katika jamii. 


HIVI PUNDE

Ghasia zatanda kwenye mkutano wa UDA Mombasa

Hali purukushani imeshuhudiwa Leo wakati wa mkutano wa wajumbe wa Chama Cha UDA kwenye kaunti ya Mombasa baada ya wafuasi wa  mbunge wa EALA...