Aug 19, 2022

SABABU ZA RUTO KUIMARIKA PWANI KATIKA UCHAGUZI MKUU

 

 

Licha ya kuwa mgombeaji wa kiti Cha Urais Kupitia  Muungano wa Azimio One Kenya  Raila Odinga amefanikiwa  kwa mara nyengine tena  kuibuka  na kura nyingi katika kanda wa pwani katika uchaguzi mkuu uliyotamatika, rais mteule William Ruto kwa upande wake amefanikiwa kupunguza pengo lilokuwa hapo awali na imani kuwa kuwa kanda ya pwani  ni ngome ya kisiasa ya Bwana Odinga.

Ruto pamoja na timu yake ya Kampeni walitumia mikakati amabayo iliwawezesha kupata  kura takriban laki 336,478 katika kaunti sita za pwani amabzo zinajumuisha  ile ya Mombasa, Lamu, Tana River, Kwale, Kilifi and Taita Taveta. Hesabu hiyo ikiwa ni Ongezeko kutoka Kura hizo ikiwa ni Ongezeko kutoka kura  287,606 ambazo chama cha Jubilee kulifanikiwa kupata katika uchaguzi wa mwaka 2017 ambao uliwapa ushindi rais Uhuru Kenyatta pamoja na Ruto.

Wadadisi wa maswala ya kisiasa wanahoji kuwa Ongezeko la Kura alizozipata Bwana Ruto Katika kanda ya Pwani  zinatokana na hatua yake ya kuwavuta  Viongozi tajika wa eneo hilo upande wake pamoja na kuandaa vikao vya kujadili maswala ya maendeleo eneo hilo ili kuwavutia wapiga kura kujifungamanisha na chama chake cha UDA.

Katika kampeni zake rais Mteule William Ruto alionekana kumshutumu vikali Mpinzani wake mkuu Raila Odinga kwa kuwatenga wafuasi wake wa kanda ya pwani jambo ambalo kulingana na wadadisi wa maswala ya kisisiasa wanasema kuwa  lilichangia pakubwa  kwa chama cha ODM kushindwa katika uchaguzi mdogo eneo bunge la Msambweni amabapo mgombeaji  kutoka chama cha UDA  Faisal Bader aliibika na ushindi.Uchaguzi huo ukiweka msingi kwa Rais Mteule William Ruto kuenziwa nawakaazi wa kanda ya pwani.  

Aug 18, 2022

SARAI AIKOSOA IEBC KUHAIRISHA UCHAGUZI WA UGAVANA

 

Mgombeaji wa kiti cha Ugavana katika kaunti ya Mombasa kupitia kwa chama cha UDA Hassan Omar Sarai ameikosoa tume huru ya Uchaguzi na Mipaka nchini IEBC kufuatia hatua yake hapo Jana kuahirisha tena uchaguzi wa Ugavana katika kaunti hiyo.

Akizungumza katika kikao na wananahabari mjini Mombasa,Sarai ameitaja hatua hiyo ya IEBC kama inayoongeza hofu miongoni mwa wakaazi wa kaunti hiyo huku akimtaka mwenyekiti wa time hiyo wafula Chebukati kuweka tarehe kamili ambapo uchaguzi huo utaandaliwa.




Wakati huo huo Sarai amewatahadharisha maafisa wa usalama dhidi ya Kutumiwa vibaya na baadhi ya wanasiasa,akisema kuwa licha ya Maafisa hao kuwahujumu, kamwe hawatalipiza kisasi huku akiwataka kutekeleza majukumu yao kulingana na katiba.


Kwa upande Mgombea mwenza wa Sarai katika kinyang’anyiro hicho Selina Maitha amewatolea wito wakaazi wa Mombasa kujitokeza kwa wingi siku ya kupiga kura na kuwapa fursa ya kuongoza kaunti hiyo Ili kuleta mageuzi ya Kimaendeleo.


HIVI PUNDE

Ghasia zatanda kwenye mkutano wa UDA Mombasa

Hali purukushani imeshuhudiwa Leo wakati wa mkutano wa wajumbe wa Chama Cha UDA kwenye kaunti ya Mombasa baada ya wafuasi wa  mbunge wa EALA...