Serikali ya kitaifa imejikita katika kuunda mkakati
wa kitaifa wa usalama wa baharini unaonuia kukabiliana na changamoto za kiusalama
zinazotokana na shughuli za uchumi samawati. Mkakati huo utakaohusisha
kamati ya kitaifa ya Usalama wa baharini na sajili ya sajili ya kitaifa ya
usalama wa baharini, ni mkakati wa kisera utakaojumuisha malengo na ruwaza ya
kuimarisha usalama wa majini katika taifa hili .
Akizungumza mjini Mombasa katika warsha ya ufunguzi wa mkakati huo ,katibu wa kudumu
katika idara ya taifa ya maswala ya Afrika Mashariki daktari Kevit
Desai,amesema kuwa mkakati huo umeundwa ili kurahisisha ushirikiano baina ya wadau pamoja na uangalizi
wa hatari na vitisho katikia sekta ya shughuli za baharini.
Aidha Desai
amebainisha kuwa uchumi samawati unashikilia nafasi ya nane miongoni mwa
mihimili ya kiuchumi katika ruwaza ya mwaka 2030 na ya tatu katika agenda nne
kuu za serikali,akisema kuwa taifa hili taifa hili limejiandaa vilivyo katika
kutekeleza jukumu muhimu la kuhakikisha usalama katika bahari hindi.
Wakati huo huo amesema kuwa ipo haja ya kulinda
usalama wa majini kutokana na vitisho vya ndani na nje ya nchi ili kuruhusu
usafirishaji wa watu na mizigo ufanyike kwa njia ya amani kwani unachangia biashara kwa asilimia tisini katika
ukanda huu.