Jun 24, 2023

Ghasia zatanda kwenye mkutano wa UDA Mombasa


Hali purukushani imeshuhudiwa Leo wakati wa mkutano wa wajumbe wa Chama Cha UDA kwenye kaunti ya Mombasa baada ya wafuasi wa  mbunge wa EALA Hassan Omar Sarai na wale wa Mbunge wa Nyali Mohammed Ali  kuonyeshana ubabe wa kisiasa.

Kizazaa kilizuka  pale mbunge wa Nyali Mohamed Ali aliposhambuliwa na watu wanaodaiwa kuwa  wafuasi wa  Hassan Omar Sarai  wakati alipowasili kwenye ukumbi wa mkutano huo, Hali iliyopekelea   kurushwa kwa vitoza machozi  na watu  wasiojukikana ili kuutawanya umati uliyokuwa umejaa ukumbini humo.



Matukio hayo yalilazimu kuhairishwa kwa mkutano huo wa wajumbe  ambao ulikuwa umeandakiwa kwa lengo la kuwahamasisha wanachama wa UDA kuhusiana na uchaguzi wa chama hicho  unaotarajiwa kuandaliwa mnamo Mwezi Agosti pamoja na kujadiliwa kwa ajenda za chama.



Hatahivyo akihutubia  wanahabari kuhusiana na matukio hayo Mbunge wa Nyali Mohammed Ali amemkosoa Hassan Omra sarai kwa madai ya kutumia vibaya nafasi yake kwenye chama UDA   ili kuhujumu matokea ya uchaguzi unaotarajiwa kuandaliwa  Mwezi Agosti.

Mbunge huyo  amemtaka Sarai kujikita katika majukumu yake kama Mbunge wa Kenya kwenye bunge la Afrika Mashariki badala ya kujihusisha na siasa za chama hicho  na kuleta migawanyiko.

Kwa upande wake Hassan Omar Sarai amemtuhumu mbunge huyo wa  Nyali kwa madai ya kughushi kadi za wajumbe waliyoalikwa kuhudhuria mkutano huo akidai  kuwa wengi wafuasi wake hakuwa  wajumbe halisi  wa UDA bali watu waliyokuwa na nia ya kuzua ghasia kwenye mkutano huo.

Wakati huo huo Sarai amepuuzilia mbali madai yaliyoibuliwa na mbunge hiyo yakumtuhumu kuwa na nia ya  kuhujumu uchaguzi wa chama hicho huku akibainisha kama naibu mwenyekiti wa chama hicho hana nia ya kufanya hivyo.

 Amekashifu ghasia zilizishuhudiwa wakati wa mkutano huo  huku akipuuzilia mbali madai kuwa analenga kuhujumu uchaguzi wa chama hicho.

Naye katibu mkuu wa chama cha UDA Cleophas Malala ambaye alikuwa amehudhuria mkutano amesisitiza Kuwa uongozi wa  chama hicho kamwe hautaegemea upande wowote katika uchaguzi unaokuja huku akiwataka viongozi hao wawili kukaa chini na kuzika tofauti zao.

Wakati huo huo amesema kuwa chama kitalazimika kuchukua hatua za kinidhamu kwa kiongozi yeyote atakayepatikana kuhisika na ghasia zilizishuhudiwa wakati wa mkutano huo.

AFUENI KWA MADEREVA WA TUK TUK MOMBASA

 Na Nyota Suleiman




MADEREVA wa Tuk Tuk katika kaunti ya Mombasa wana kila sababu ya kutabasamu baada ya kampuni ya Car General Kuzindua rasmi aina mpya za Tuk Tuk PIAGGIO NXT zenye Muundo wa kipee ambazo zinatarajiwa kupiga Jeki biashara hiyo na kuiboresha zaidi katika kaunti hiyo.

Uzinduzi wa aina hiyo mpya ya Tuk Tuk  unajiri kufuatia malalamiko kutoka kwa madereva wa Tuk Tuk kuhusiana na mapungufu yaliyoshuhudiwa katika Tuk Tuk za  hapo awali zilizonunuliwa kutoka kwa kampuni hiyo.

Kulingana na raisi wa Muunganao wa madereva wa Tuk Tuk kaunti ya Mombasa ambaye pia ni mwanzilishi wa biashara hiyo katika kaunti  hiyo Chrispine Obondo maarufu Mr Dubai ameutaja uzinduzi huo kama hatua muhimu katika sekta ya uchukuzi katika kaunti ya Mombasa akisema itawasaidia pakubwa madereva wa Tuk Tuk  kumudu gharama ya biashara hususan bei ya mafuta kutokana na muundo  wa Kipekee wa Tuk Tuk Hizo.

Wakati huo huo ameipongeza kampuni ya Car and general kwa kutoa kipaumbele katika kuangazia maslahi na matatizo yanayowakumba Madereva na kutafuta suluhu muafaka ili Kuwawezesha kuendeleza biashara bila madhila yoyote.

Aidha  ametoa wito kwa madereva wa Tuk Tuk katika kaunti ya Mombasa kupewa mafunzo ya Kutosha kuwawezesha kuendeleza shughuli zao ipasavyo ili  kuwaepushia mahangaiko wanayopitia kutoka kwa maafisa trafiki katika kaunti hiyo.

Wakati huo huo ameonyesha kusikitishwa kwake na jinsi baadhi ya maafisa hao wa trafiki wamekuwa wakiwahanagaisha madereva wa tuk tuk bila  hatia ,akiwataka kukomesha hujuma dhidi yao.

Baadhi ya Madereva waliyozungumza katika hafla ya Uzinduzi huo iliyoandaliwa katika uga wa Makadara mjini Mombasa Wameonyesha furaha yao kutokana ujio wa Tuk Tuk hizo mpya huku wakiwarai wenzao kujiunga na miungano ya madereva ili wawaze kujinufaisha zaidi.

Kwa upande wao maafisa kutoka kampuni ya Car and general   waliyohudhuria uzinduzi huo wamewahimiza madereva kujitokeza na kuchukua mikopo ya kununua Tuk Tuk hizo mpya ili waweze kujiendeleza zaidi kichumi.


HIVI PUNDE

Ghasia zatanda kwenye mkutano wa UDA Mombasa

Hali purukushani imeshuhudiwa Leo wakati wa mkutano wa wajumbe wa Chama Cha UDA kwenye kaunti ya Mombasa baada ya wafuasi wa  mbunge wa EALA...